-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Monday 21 July 2014

WAGANGA NA WATABIBU TIBA ASILI WAASWA WASIRUBUNIWE




UONGOZI wa Umoja wa Waganga na Watabibu wa Tiba asili nchini umewataka watabibu wa tiba asili kujiunga na vyama vya waganga ili kufahamika kama watoa huduma katika maeneo wanayoishi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Umoja huo Bw.Simba Abrahman wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye kikao cha makabidhiano ya fomu za usajili wa watabibu hao.

Bw.Abrahman amesema kuwa mpaka sasa watabibu 33 wameshajiandikisha kuchukua fomu za usajili kama agizo la Waziri Mkuu linavyosema sambamba na sheria ya Tiba Asili inavyotaka.

Aidha amewataka watabibu kutokubali kurubuniwa na kupewa vyeti feki bila kufata hatua zinazotakiwa ikiwa ni pamoja na kupeleka fomu kuthibitishwa na mjumbe wa mahali anapoishi.

“natoa wito kwa watu wasije kudanganyika na kupewa vyeti feki bila kufuata hatua zinazotakiwa ,tutashirikiana na wenzetu kuhakikisha waganga wote wanaotoa huduma wamesajiliwa na wanavibali.”Alisema Abrahaman

Ameongeza kuwa watabibu wenye mabango barabarani yanayoeleza magonjwa wanayotibu hawanabudi kuyatoa na kuweka mabango mapya kwani yanakiuka sheria ya Tiba asili ambayo inataka mtoa huduma hiyo kutaja jina lake , mahali anapopatikana na namba ya simu.

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *