-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Wednesday 30 July 2014

Ajali yaua watu 17 Tanzania

Moja ya ajali ya magari ya abiria
Watu 17 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea mkoa wa Dodoma katikati mwa Tanzania.
Taarifa zinasema ajali hiyo imetokea baada ya magari mawili, moja lori na jingine basi la abiria kugongana uso kwa uso.
Akizungumza na BBC Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma David Misime amesema ajali hiyo iliyotokea majira ya saa mbili za asubuhi siku ya jumatano imesababishwa na kile kinachodaiwa kuwa uzembe wa dereva la gari moja lililohusika katika ajili hiyo.
Amesema ajali hiyo ilihusisha basi la abiria na Lori ambayo yaligongana uso kwa uso baada ya dereva wa lori kujaribu kulipita gari jingine bila kuangalia vizuri na hivyo kujikuta yakigongana.
Tayari polisi wa Tanzania wameanza uchunguzi ili kujua chanzo cha ajili hiyo lakini hata hivyo imeshindwa katika hatua za awali kumshikilia mtu yoyote kwa vile maderava na magari yote ni miongoni mwa walikufa katika ajali.
Hii si mara ya kwanza kwa ajali kama hii kutokea hapa Tanzania ambapo sababu kadhaa zimekuwa zikitajwa kusababisha ikiwemo mwendo kasi wa magari, uzembe wa madereva, pamoja na ubovu wa barabara

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *