-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Friday 28 November 2014

ELIMU KWA JAMII JUU YA AINA ZA WAGANGA NA BORESA TRADITIONAL MEDICINE COMPANY LTD.


Katika swala la utoaji elimu kwa Jamii, elimu juu ya Tiba Asili inafaa itolewe na Waganga wa Asili wenyewe ili kuweza kubadilisha Imani zinazowapotosha wanajamii hata kufikia kutendeana maovu yanayopelekea mauaji. Elimu hii si vyema ikatolewa na Watu wengine kama Vile Maaskofu, Masheikh, Wanasheria, Madaktari wa Kisasa, Wanasiasa n.k kwa kuwa Jamii haitapokea ujumbe wao Kirahisi kwani wamezoeleka kwa Kazi zingine siyo kwa Kazi hiyo ya Imani za ushirikina na uchawi
Katika Imani ya kawaida Kuna Aina za waganga kama ifuatavyo
                              I.            Waganga wa Asili
                           II.            Waganga wa Jadi
                        III.            Waganga wa Kienyeji

1.    WAGANGA WA ASILI.
Mganga wa Asili ni yule anayeshughurika na Tiba za Maradhi kwa Kutumia dawa zaAsili ili kuondoa Maradhi yanayosumbua Jamii iwe kwa Binadamu, wanyama, mimea n.k kwa Kufuata maadili ya utoaji huduma ya Utabibu

2.    WAGANGA WA JADI.
Mganga wa Jadi ni yule anaetumia Mila na Desturi katika Tiba na Utoaji wa dawa kwa wagonjwa iwe Binadamu, Wanyama, Mimea n.k. hivyo hutegemea Zaidi Mila na Desturi kama kanuni na maadili ya utoaji wa Huduma ya Tiba.

3.    MGANGA WA KIENYEJI.
Mganga wa Kienyeji ni Yule Ambaye hana Mafunzo Maalum ya Tiba ya Upande wowote maalum wa tiba  ya Upande wowote katika utoaji wake huduma kwa jamii. Ni mtu anayeweza kuchanganya taaluma mbalimbali hata za kisayansi ili mradi afanikishe alichokusudia. Mganga huyo pia anaweza kutumia vazi lolote liwe la sheikh, askofu, daktari, Mganga wa asili n.k ili mradi atimize alokusudia. Mganga yeyote mwenye fani nzuri akiitumia katika kutenda maovu hufahamika kama mganga wa Kienyeji katika Tiba za Asili.

je Huyu ni Aina gani ya Mganga?

Thursday 27 November 2014

NA HIVI NDIVYO MAONYESHO YA KWANZA YA KIMATAIFA YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA YALIVYOKUWA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

WATAALAMU WA TIBA ASILI WAKUTANA CHINI YA JUKWAA MOJA; WAONYESHA UMAHIRI KATIKA TIBA ASILI NA MBADALA

Mratibu wa Jukwaa la Tiba Asili Tanzania, Boniventura F. Mwalongo akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja yalikofanyika Maonyesho ya Tiba Asili na Mbadala


Dr. Jumanne wa Huduma ya Uponyaji akimsikiliza mmoja wa waliotembelea Banda lake kwenye Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Tiba  zinazotolewa na Dk. Jumanne ni zile zinazotokana na Matunda na Mboga Mbalmbali . Simu 0755087303





Dk. Salimu akiwaeleza watu waliofika kwenye maonyesho ya dawa asili jinsi dawa zake zinavyofanya kazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja


Dk.Ahmad Darusi Salimu Mkurugenzi wa M. M.D.K Clinic akitoa maelezo ya jinsi dawa zake zinavyotakiwa kutumika. Yeye amebobea katika kutibu Kansa za aina zote na pia anayo dawa inayosaidia kuondoa magonjwa nyemelezi kwa wagonjwa wa UKIMWI. Simu 0754467406, 0787467406

Mkurugenzi wa Kampuniya Dk.Fadhili Herbal Medicine & Nutritional,akitoa maelezo kwa wateja ((hawapo pichani) waliofika kwenye Banda lake wakati wa Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala yaliyofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja hivi Karibuni.  Dk. Fadhili pia ni Mshauri wa Afya katika Kampuni ya BF SUMA kutoka Marekani inayojishuhulisha na usambazaji wa dawa zenye Virutubisho vinavyoweza kuongeza kinga ya mwili (CD4) kwa 100%, kurekebisha Sukari na zingine nyingi.  Simu 0713834556

Dk. Nyakubaho (katikati) Mkurugenzi wa Kikundi cha tiba Asili cha Nyakiziba Shunga Tradtional Clinic. Wanazo dawa nyingi za kutibu maradhi mbalimbali kama inavyoonekana Pichani. Simu 0784936177, 0755570321

Bi EmilianaKokuhumuliza, Mtabibu wa asili anayetibu kwa kutumia mitishamba kutoka Mkoa wa Kagera. anapatikana Mjini Morogoro. Simu 0766903297. Picha zote na Muchunguzi Kamugisha wa ZUNGU

mhe.Kingunge Ngombale Mwilu akitembelea moja ya mabanda katika maonesho ya kwanza ya kimataifa ya tiba asili ya mwafrika

























































MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *