-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Thursday 23 June 2016

WATU WENYE UALBINO WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA KUJENGA UELEWA KUHUSU ALBINO


 Watanzania wakishiriki kwenye matembezi ya Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu Albino kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo Juni 13, 2016. Baraza la Usalama la Umoja wa Matifa liliitangaza tarehe 13 ya kila mwaka kuwa iwe Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu watu wenye Ualbino kwa nia ya kuondoa unyanyapaa, ukatili dhidi yao na kujenga heshima ya utu wa mtu.(PICHA ZOTE NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID)
  Watanzania wakishiriki kwenye matembezi ya Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu Albino kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo Juni 13, 2016. Baraza la Usalama la Umoja wa Matifa liliitangaza tarehe 13 ya kila mwaka kuwa iwe Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu watu wenye Ualbino kwa nia ya kuondoa unyanyapaa, ukatili dhidi yao na kujenga heshima ya utu wa mtu
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu), Dkt. Abdallah Posii, akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja kuongoza siku hiyo.
 Mtoto wa darasa la kwanza wa shule ya Jeshi la Uokovu, jijini Dares Salaam, Happy Simon (9), akilia baada ya kuimba wimbo unaotoa elimu kwa jamii kuwapenda na kuwalinda watoto wenye ualbino
 Dkt. Possi akimnyanyua mtoto Happy baada ya kuimba wimbo wake ambao ulisisimua wengi na kuinua hisisa kali
 Mmoja wa watu wenye ualbino, akisakata rhumba kutoka bendi ya Akudo Impacte waliokuwa na jukumu la kuburudisha hadhira
 Mfumaji mahiri wa kutumia shanga, Sophia Mohammed, (kushoto0, akimpatia maelezoNaibu Waziri Dkt. Possi (mwenye kofia) kuhusu ufundi wake na jinsi anavyojipatia kipato kwa kazi hiyo
 Mtoto huyu ni miongoni mwa watoto wengi waliohudhuria hafla hiyo
 Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake, wakati wakiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
 Mama huyu akiwa na mtoto wake mwenye ualbino ni miongoni mwa waliohudhuria sherehe hiyo
 Afisa Mkuu Mtendaji wa Under The Same Sun, (UTSS), taasisi ya Kimataifa inayojishughulisha na utetezi wa watu wenye ualbino, Bi. Vicky Ntetema, (kulia), akifurahia jambo na wadau wake
 Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake kwenye sherehe hizo
  Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake kwenye sherehe hizo

Mama huyu akisubiri watu watembelee kwenye bidhaa zake
 Mtoto mwenye ualbino akishiriki matembezi hayo na mama yake
 Balozi wa Canada nchuini Tanzania, Alexandre Levique, (kushoto), Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dkt. Reginald Mengi, (wapili kulia), na Maria Stanford, wakimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu, wa Shirika la Kimataifa linalotetea watu wenye Ualbino, Under The Same Sun (UTSS), Bi. Vicky Ntetema, wakati wa maadhimisho hayo
 Naibu Waziri Dkt. Possi naviongozi wengine kwenye meza kuu wakipokea matembezi ya maadhimisho ya sikuya kimataifa wa kujenga uelewa kwa watu wenye ualbino
Bi Ntetema (kulia), akitembelea moja ya mabanda ya biadhaa zinazotengenezwa na kuonyeshwa na watu wenye ualbino pamoja na wadau wengine

Friday 10 June 2016

Rais Maguifuli atarajiwa kuwa mgeni rasmi siku ya Kimataifa ya Albino.

Rais Maguifuli atarajiwa kuwa mgeni rasmi siku ya Kimataifa ya Albino.

Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu ualbino yatakayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam. Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama cha Watu Wenye Ualbino Nchini (Tanzania Albinism Society) Nemes Temba ameeleza kuwa kupitia maadhimisho hayo jamii itapata fursa ya kupewa elimu muhimu kuhusu ualbino ili kuondoka na dhana potofu hususani ushirikina. “Maadhimisho haya ambayo yataanza Juni 11 hadi Juni 13, 2016 yatasindikizwa na mambo mbalimbali ikiwemo huduma za afya hususani uchunguzi na matibabu ya saratani ya ngozi pamoja na nasaha za viongozi na mabalozi, utambulisho wa Miss Albino Tanzania na uzinduzi wa kamusi ya ulemavu,” alisema Temba. Temba aliendelea kuainisha kwamba siku hiyo itawapa fursa watoto wenye ualbino waishio kwenye vituo mbalimbali nchini kutembelea mji wa Bagamoyo kujionea mambo mbalimbali chini ya ufadhili wa shirika la UNICEF. Aidha Mwenyekiti huyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwapa vipaumbele watu wenye ulemavu akiwemo Dkt. Abdallah Possi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Ajira, Kazi na Watu Wenye Ulemavu hii inadhihirisha kuwa ulemavu si hoja bali utendaji kazi ndio kitu umuhimu. Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wenye Alibinism Tanzania (TAS) Nemes Temba akizungumza na waandishi wa Habari (hawapopichani) leo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujulisha umma siku ya maadhimisho ya Albino duniani.Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa TAS Dar es Salaam, Gabriel Aluga, Katibu Mkuu wa TAS, Musa Katimba na Mratibu kutoka asasi ya kiraia ya BADEF. Mwenyekiti wa Mfuko wa Good Hope Star na mjumbe wa kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Albino duniani Al Shamaymaa Kwegyir akifafanua jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa Habari (hawapopichani) leo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujulisha umma siku ya maadhimisho ya Albino duniani.Kutoka kuliani Mwenyektiwa TAS Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TAS, Musa Katimba (kushoto) na Mwenyekiti wa TAS Taifa Nemes Temba.

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *