-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Thursday 23 June 2016

WATU WENYE UALBINO WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA KUJENGA UELEWA KUHUSU ALBINO


 Watanzania wakishiriki kwenye matembezi ya Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu Albino kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo Juni 13, 2016. Baraza la Usalama la Umoja wa Matifa liliitangaza tarehe 13 ya kila mwaka kuwa iwe Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu watu wenye Ualbino kwa nia ya kuondoa unyanyapaa, ukatili dhidi yao na kujenga heshima ya utu wa mtu.(PICHA ZOTE NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID)
  Watanzania wakishiriki kwenye matembezi ya Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu Albino kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo Juni 13, 2016. Baraza la Usalama la Umoja wa Matifa liliitangaza tarehe 13 ya kila mwaka kuwa iwe Siku ya Kimataifa ya Kujenga Uelewa kuhusu watu wenye Ualbino kwa nia ya kuondoa unyanyapaa, ukatili dhidi yao na kujenga heshima ya utu wa mtu
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu), Dkt. Abdallah Posii, akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja kuongoza siku hiyo.
 Mtoto wa darasa la kwanza wa shule ya Jeshi la Uokovu, jijini Dares Salaam, Happy Simon (9), akilia baada ya kuimba wimbo unaotoa elimu kwa jamii kuwapenda na kuwalinda watoto wenye ualbino
 Dkt. Possi akimnyanyua mtoto Happy baada ya kuimba wimbo wake ambao ulisisimua wengi na kuinua hisisa kali
 Mmoja wa watu wenye ualbino, akisakata rhumba kutoka bendi ya Akudo Impacte waliokuwa na jukumu la kuburudisha hadhira
 Mfumaji mahiri wa kutumia shanga, Sophia Mohammed, (kushoto0, akimpatia maelezoNaibu Waziri Dkt. Possi (mwenye kofia) kuhusu ufundi wake na jinsi anavyojipatia kipato kwa kazi hiyo
 Mtoto huyu ni miongoni mwa watoto wengi waliohudhuria hafla hiyo
 Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake, wakati wakiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam
 Mama huyu akiwa na mtoto wake mwenye ualbino ni miongoni mwa waliohudhuria sherehe hiyo
 Afisa Mkuu Mtendaji wa Under The Same Sun, (UTSS), taasisi ya Kimataifa inayojishughulisha na utetezi wa watu wenye ualbino, Bi. Vicky Ntetema, (kulia), akifurahia jambo na wadau wake
 Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake kwenye sherehe hizo
  Mama huyu mwenye ualbino akiwa amembeba mtoto wake kwenye sherehe hizo

Mama huyu akisubiri watu watembelee kwenye bidhaa zake
 Mtoto mwenye ualbino akishiriki matembezi hayo na mama yake
 Balozi wa Canada nchuini Tanzania, Alexandre Levique, (kushoto), Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dkt. Reginald Mengi, (wapili kulia), na Maria Stanford, wakimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu, wa Shirika la Kimataifa linalotetea watu wenye Ualbino, Under The Same Sun (UTSS), Bi. Vicky Ntetema, wakati wa maadhimisho hayo
 Naibu Waziri Dkt. Possi naviongozi wengine kwenye meza kuu wakipokea matembezi ya maadhimisho ya sikuya kimataifa wa kujenga uelewa kwa watu wenye ualbino
Bi Ntetema (kulia), akitembelea moja ya mabanda ya biadhaa zinazotengenezwa na kuonyeshwa na watu wenye ualbino pamoja na wadau wengine

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *