-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Monday 19 September 2016

TRAMEPRO yaandaa mafunzo kwa watoa Tiba Asili

Shirika la Dawa Asili na Ulinzi wa Mazingira nchini Tanzania – TRAMEPRO, limeandaa mafunzo kwa watoa tiba asili na tiba mbadala kutoka maeneo yote nchini.




Katibu Mkuu wa TRAMEPRO, Bw. Boniventura Ferdinand Mwalongo

Lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa watoa tiba asili na tiba mbadala wanafanya shughuli zao kwa kufuata kanuni, sheria na taratibu ili kundoa misuguano isiyo na lazima baina yao na wasimamizi wa sheria.
Katibu Mkuu wa TRAMEPRO Bw. Boniventura Mwalongo amesema hayo jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuifanya tiba asili nchini kutolewa katika viwango vinavyokubalika na hivyo kuwapa Watanzania huduma bora za tiba asili.
Kuhusu msadaa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililoikumba mikoa ya Kanda ya Ziwa; Afisa Uhusiano wa shirika hilo Bw. Alberto Sanga amewataka wadau wa mazingira na Watanzania kwa ujumla kushirikiana na serikali katika kuchangia wahanga wa tukio hilo alilosema kuwa chanzo chake ni cha asili na kwamba hakitokani na sababu za kibinadamu.

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *