-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Friday 5 September 2014

Utata kauli za Serikali ya kupiga marufuku matangazo ya tiba asili

  
masomo-bango-mganga
MABANGO ya matangazo ya waganga wa jadi yanaikoroga serikali kutokana na mara kadhaa kutoa maagizo ya kuyapiga marufuku bila mafanikio yoyote.
Taarifa zilizoifikia FikraPevu zimeeleza kwamba agizo hilo la mara kadhaa bila kutekelezwa kutokana na kauli hizo kutolewa bila ufuatiliaji katika kipindi cha miaka minne hadi sasa.
Aidha, licha ya serikali kutoa kauli hizo kupitia vyombo vya habari na Bunge, mabango ya wataalamu hao yanayojitangaza kutibu maradhi sugu yameelezwa kuwakera baadhi ya wananchi katika maeneo mbalimbali nchini kutokana na serikali kushindwa kutatua tatizo hilo.
Imebainika kuwa tangu tamko hilo kutolewa na serikali mwaka 2010 mabango hayo yameendelea kuwekwa zaidi katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mbeya, Tanga, Kigoma, Pwani, na mikoa ya kanda za juu kusini na kati bila serikali kuchukua hatua stahiki dhidi yao.
mmalawi-mganga-bango-kiboko
Matukio ya kishirikiana
Katika mtandao wa kuaminika wa kijamii wa JamiiForums kumekuwepo na mjadala wa matangazo hayo na kuwa mabango hayo hayalipiwi kodi licha ya wakati mwingine kuwekwa kwenye nguzo za umeme kinyume cha sheria.
mganga-freemason
Wamesema matukio ya mauaji yanayotokea katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo mkoa wa Mara na mikoa ya Kanda ya Ziwa, yanasababishwa na imani za kishirikiana kutokana na mabango hayo ambayo hueleza kutibu magonjwa sugu pamoja na kupandishwa cheo makazini na utajiri.
Utapeli kwa njia ya mabango
Mjadala huo umelalamikia hatua ya mabango hayo kuachwa yakijitangaza bila kulipa kodi.
“Sasa hivi Tanzania kuna staili mpya ya kupata fedha, huhitaji kutumia nguvu bali ni kucheza na akili ya mtu kwani kila unapopita utakuta tangazo la mganga wa kienyeji na wanaweka na namba za simu na kila mganga anaandika anatoka Sumbawanga, Tanga, Kigoma, au Pemba,” anaeleza mchangiaji mmoja wa JamiiForums.
DrMkombozi-cheo-kazini
Hata hivyo, wamesema mikoa ambayo imekithiri kwa zoezi hilo ni Dar es Salaam, Arusha, Mbeya, Tanga, Kigoma, Pwani, na mikoa ya kanda za juu kusini na kati.
Kauli ya Serikali isiyotekelezeka
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, jana Jumanne Juni 3, 2014 alisema serikali imetangaza kuondolewa haraka mabango hayo kwa kile alichodai kuwa kuendelea kujitangaza kwa watu hao kutibu maradhi sugu ikiwemo Ukimwi, Shinikizo la damu na kisukari ni kosa kwa mujibu wa sheria.
Amesema Wizara hiyo, itatoa muongozo na taratibu zinazopaswa kufuatwa hivi karibuni, ili dawa husika ziweze kukaguliwa na kupimwa kitaalamu bila ya kutumiwa na wahusika.
Tafiti za waganga wa kienyeji
Hivi karibuni Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu NIMR, ilieleza kuanza mkakati utakaowezesha uhakiki wa dawa za waganga wa tiba asili nchini, ili kudhibiti viwango na afya za watumiaji.
Taarifa ya NIMRI ilisema hatua hiyo itawezesha kuhakikiwa kwa madawa ya waganga wa tiba mbadala ambao wamekuwa wakitoa huduma za kitabibu katika maeneo mbalimbali hapa nchini.  
Waganga wa tiba za jadi nchini, wamekuwa wakilalamikiwa mara kwa mara na wananchi wakiwataka kuacha kuwadanganya watu kuwa wanatibu magonjwa kama kifua kikuu, kisukari na Ukimwi kwa kuwa sheria haziwataki kujitangazana, licha ya baadhi yao kuendelea kutumia kutumia yiba hizo.
Kwa upande wa Kambi ya Upinzani Bungeni, imeitaka serikali kuwafutia vibali vya biashara, wafanyabiashara wanaoingiza vipodozi venye kemikali vilivyopigwa marufuku na mamlaka husika hapa nchini.
Wakichangia hotuba ya bajeti ya wizara hiyo, baadhi ya wabunge wamelalamikia hatua ya kitendo cha serikali kutoa asilimia 48 ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge kwa mwaka wa fedha 2013/2014 licha ya umuhimu wa wiizara hiyo kubeba maisha ya Watanzania.

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *