-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Friday 22 August 2014

CCM, UKAWA HAKUNA MBABE’

Viongozi wa Chama cha ukawa wakijadili jambo.
Na mwandishi wetu.
SAKATA la kuendelea au kutoendelea kwa Bunge Maalum la Katiba linalofanya vikao vyake mjini Dodoma, limeelezwa kuwa halitakuwa na mshindi endapo hakutakuwa na maridhiano baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Ijumaa limeambiwa.
Wakihojiwa kwa nyakati tofauti kufuatia kauli ya Katibu wa Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kudai kuwa chama chao kimebariki mchakato kuendelea, baadhi ya wananchi wamesema msimamo huo una faida na hasara zake kwa vile kinachotafutwa, si masilahi ya makundi hayo mawili pekee.
“Kuna mambo mengi sana ya msingi kwa Watanzania yanayotakiwa kujadiliwa katika katiba kuliko vitu vidogo vinavyowagawa hawa waheshimiwa, sasa hapa kunatakiwa maridhiano ya dhati ili katiba itakayopatikana isiwe na makengeza,” alisema Mwarami Jones, wa Dodoma, alipotoa maoni yake kwa njia ya simu.
Darren Pusa, msomi wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi, alisema kisheria mchakato unaoendelea mjini Dodoma ni halali kwa vile kila kitu kipo kwa mujibu wa sheria, lakini kitakachotia doa ni katiba hiyo kuonekana kuandikwa na chama kimoja ambacho ni tawala.
“Inapoonekana kwamba CCM ndiyo inayoandika katiba, hiyo ni dosari, hata kama kuna vyama vidogovidogo vilivyobaki bungeni. Tatizo hapa kila mmoja anataka kuonyesha ana nguvu, mwisho wa siku Watanzania ndiyo wanaumia, vita hii haina mbabe,” alisema na kuziomba pande hizo mbili kufikiria kukaa mezani.
Jumanne na Jumatano Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi ilikutana mjini Dodoma kuzungumzia maendeleo ya mchakato wa katiba, wakati huu Ukawa ikiwa imesisitiza kuwa haitarejea bungeni kama Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Jaji Warioba haitajadiliwa.

0 comments:

Post a Comment

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *