-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Monday, 19 September 2016

TRAMEPRO yaandaa mafunzo kwa watoa Tiba Asili

Shirika la Dawa Asili na Ulinzi wa Mazingira nchini Tanzania – TRAMEPRO, limeandaa mafunzo kwa watoa tiba asili na tiba mbadala kutoka maeneo yote nchini.




Katibu Mkuu wa TRAMEPRO, Bw. Boniventura Ferdinand Mwalongo

Lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa watoa tiba asili na tiba mbadala wanafanya shughuli zao kwa kufuata kanuni, sheria na taratibu ili kundoa misuguano isiyo na lazima baina yao na wasimamizi wa sheria.
Katibu Mkuu wa TRAMEPRO Bw. Boniventura Mwalongo amesema hayo jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa mafunzo hayo yatasaidia kuifanya tiba asili nchini kutolewa katika viwango vinavyokubalika na hivyo kuwapa Watanzania huduma bora za tiba asili.
Kuhusu msadaa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililoikumba mikoa ya Kanda ya Ziwa; Afisa Uhusiano wa shirika hilo Bw. Alberto Sanga amewataka wadau wa mazingira na Watanzania kwa ujumla kushirikiana na serikali katika kuchangia wahanga wa tukio hilo alilosema kuwa chanzo chake ni cha asili na kwamba hakitokani na sababu za kibinadamu.

Saturday, 10 September 2016

TAMKO LA KATIBU MKUU WA TRAMEPRO KUHUSU WATOTO WALIOMALIZA ELIMU YA MSINGI LILILOTOLEWA TAREHE 10/09/2016

TRADITIONAL MEDICINE AND ENVIRONMENTAL PROTECTION
SHIRIKA LA DAWA ASILIA NA ULINZI WA MAZINGIRA




TAMKO LA KATIBU MKUU WA TRAMEPRO KUHUSU WATOTO WALIOMALIZA ELIMU YA MSINGI LILILOTOLEWA TAREHE 10/09/2016

Ndugu Waandishi wa Habari,

Katika jamii yoyote ile duniani watoto wote bila kujali kabila, mila, rangi, utaifa,dini, jinsia, ulemavu, hali ya kiuchumi, ukimbizi au hali yoyote , moja ya haki na urithi pekee wenye thamani kwao ni Elimu. Elimu humfanya mtoto aweze kujitambua na kumpa upeo utakaomuwezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha ili aweze kuishi vyema katika maisha yake ya hapa duniani.

Nitumie fursa hii kuwapongeza watoto wote waliomaliza mtihani wa Taifa wa kuhitimu Elimu ya Msingi mwaka huu wa 2016, PONGEZI SANA! Ni jambo muhimu kama wazazi/ walezi na Taifa kwa ujumla kwani hii ni fursa adimu kwa ustawi na maendeleo ya mtoto na ni miongoni mwa njia ya kutimizwa kwa haki ya msingi ya mtoto ya kuendelezwa ambayo inamjengea mtoto msingi imara wa maisha yake ya baadae.

Ndugu Wanahabari, TRAMEPRO tunaipongeza Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwani Takwimu zinaonyesha kuwa, wanafunzi 795,761 (wavulana 372,883 sawa na asilimia 46.86 na wasichana 422,878 sawa na asilimia 53.14) wamesajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka huu.

Ni matarajio yetu kuona watoto wote wanapata nafasi ya elimu ya Sekondari kwakuwa Msingi tayari umeshawekwa na Serikali yetu tukufu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wa kutoa na imekusudia kumpa kila mtoto Elimu ya Sekondari bure. Hivyo tusingefurahi mmojawapo kati ya watoto hawa waliomaliza elimu ya msingi akaikosa nafasi hii kwa sababu zinazoweza kuzuilika

Hivyo ningependa kutumia fursa hii pia kuwaasa watoto waliomaliza darasa la saba kutojihusisha na tabia au vitendo vyovyote vinavyo hatarisha afya, usalama na maendeleo yao, kama vile kujihusisha kwenye masuala ya ngono, matumizi ya madawa ya kulevya na vileo katika kipindi hiki cha kusubiri matokeo ya mitihani yao.

 Watoto wetu wa Kike na Kiume wajitambue, na wajue kuwa wao ni hazina ya pekee katika maendeleo ya nchi yetu. Kipindi hiki wakitumie vizuri kwa kuwa waadilifu, waaminifu, wenye bidii na kuzingatia kanuni za nidhamu na tabia njema huku wakijiandaa kwa ajili ya kuendelea na elimu ya Sekondari.


Ndugu waandishi

Pamoja na juhudi nzuri ya serikali ya kuhakikisha elimu inapatikana bure kwa watoto wote kuanzia shule ya msingi hadi sekondari, lakini bado kunawananchi wengi hawajapata elimu nzuri na yakutosha kwa kuhusha elimu na mambo ya ushirikina. Hari hiyo hupelekea kukwamisha maendeleo ya elimu kwa watoto na hasa maeneo ya vijijini
Kwa waganga wachache wasiokuwa waaminifu wasiofuata maadili katika utabibu kuihusisha tiba asili na ushirikina. Hali ambayo huchochea umasikini na kukwamisha maendeleo ya elimu

TRAMEPRO inapenda kuwaasa wazazi, walezi na watoto
kuwaasa watoto wote kutumia kipindi hiki kwa kukataa kurubuniwa, kushawishiwa na kujiingiza katika mambo yenye kuhatarisha afya, usalama na maendeleo yao.

TRAMEPRO inawataka Wazazi Walezi Watoto na jamii kwa ujumla:-

1.  Kuwashirikisha watoto katika shughuri mbalimbali za usafi na ulinzi wa mazingira katika kipindi hiki cha kusubiria matokeo yao na isiwe Kuwaozesha watoto wa wao waliohitimu darasa la saba kwa sababu yoyote ile au kwa lengo la kujipatia mali kwa njia ya mahari.

2.  Kuwashirikisha watoto kupata maoni yao, kujiunga na vikundi mbalimbali vya stadi za maisha, kama michezo  kusikilizwa na kushiriki kwa hiari yake katika maamuzi yahayohusu maisha yake kulingana na umri na upeo wake.

3.  Kuwapa uhuru watoto wa kujifunza asili yao, tamaduni zao kwa kuwaelimisha kutofuata matembo mabaya yanayofanywa na baadhi ya wanajamii kwa mfano kujiepusha na jamii zenye Imani potofu kama unyanyapaa kwa watu wenye ualbino.

4.  Kuwaasa watoto kujiepusha na kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi wakiwa na umri mdogo pamoja na kuwapa elimu juu ya magonjwa ya kuambukiza na mimba katika umri mdogo.  Kwa mujibu wa Sheria ya makosa ya kujamiiana ya mwaka 1998 ambayo imefanyiwa marekebisho na kuhuishwa kwenye Makosa ya Jinai (Penal Code Cap 16)  inaelekeza kuwa ni kosa la jinai  kwa mtu yoyote kumlaghai mtoto wa umri wa chini ya miaka  18 kwa kumpa mimba au kufanya nae mapenzi.

5.  Pia tunapenda kuwaasa watoto kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kwa wazazi kutotoa fursa kwa watoto kutumia vibaya mitandao ya kijamii

Lengo ni kuona jamii ya watanzania inafikia malengo yake kwa kutokomeza umaskini, ujinga na maradhi kwa kuwatimizia watoto haki ya elimu ili waweze kutimiza ndoto zao na kulijenga taifa letu la Tanzania


Imetolewa na:-

BONIVENTURA F. MWALONGO
KATIBU MKUU WA TRAMEPRO
DAR ES SALAAM

10/09/2016

Thursday, 1 September 2016

TRAMEPRO YAUNGANA NA SERIKALI KATIKA MAADHIMISHO YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA KWA NCHI 46 ZA AFRIKA - WHO-AFRO

Shirika la Dawa Asilia na ulinzi wa mazingira TRAMEPRO. Tanzania Bara TUNAUNGANA NA SERIKALI,KATIKA NCHI 46 BARANI AFRIKA KUADHIMISHA SIKU YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA Tarehe 31/08/2016.Bara la Africa WHO-AFRO.UJUMBE Maalum wa mwaka huu ni "Kanuni za udhibiti wa bidhaa za Tiba Asili Katika Kanda ya Afrika" Mganga wa Tiba Asili zingatia Sera,Sheria,Kanuni ,Taratibu na Miongozo inayo simamia huduma ya Tiba Asili.TAMKO LA KATIBU MKUU KUHUSU MAADHIMIMISHO YA SIKU YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA lililotolewa 31/08/2016.KATIKA UKUMBI WA WAZIRI WA AFYA MAENDELEO YA JAMII ,JINSIA ,WAZEE NA WATOTO.
picha ni kumbukumbu mbalimbali za maonesho ya Tiba asili ya Mwafrika yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam - TANZANIA Mnamo mwaka 2014.




Tuesday, 23 August 2016

TIBA ASILIA NA TIBA MBADALA TANZANIA NA SHIRIKA LA DAWA ASILIA NA ULINZI WA MAZINGIRA TANZANIA (TRAMEPRO)

TRAMEPRO ni Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (Traditional Medicine and Environmental Protection Organization) lililosajiliwa chini ya Sheria ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali yaani Non – Govermental Organization (NGO’s) “Act 24 of 2002” lenye namba ya usajili 00NGO/00007772 linalofanya kazi kwa Karibu na Serikali na Jamii katika kufuatilia Matumizi sahihi ya dawa asilia , uandaaji wa dawa asilia, upatikanaji wa dawa asilia na uvunaji endelevu utakao pelekea kukua kwa pato la mtu mmoja mmoja na uchumi wa nchi pamoja na kulinda Mazingira ili kupata dawa asili iliyo na Virutubisho vya kutosha . Uvunaji makini wa Miti dawa utatuletea upatikanaji wa mvua za kutosha zitakazo tuwezesha katika kilimo, hewa safi, chakula pia kulinda na kuendeleza BAONUAI.
Image result for tiba asiliDira ni kuwa na Jamii yenye kuheshimu, kutumia na kulinda Dawa za Asilia zinazotoka katika mazingira Asili na yaliyolindwa, ili kutuwezesha kuwa na Afya bora, kupambana na adui maradhi nakutambua vyanzo vinavyoweza kuchafua matumizi yetu Salama na kulinda usalama wa watumiaji.
Kwapamoja tunawajibu mbalimbali katika kuangalia upatikanaji na upandaji wa miti dawa ili kupata dawa kwa wingi na kuendelea kulinda Afya zetu na kutunza mazingira yetu. TRAMEPRO tunafanya juhudi mbalimbali za kuhakikisha jamii inapata elimu ya matumizi ya dawa asili na faida zinazopatikana kwa kulinda mazingira yetu .Ili kufanikisha matumizi sahihi ya Dawa asilia na kulinda Mazingira ni muhimu Kutoa Elimu na kuwajengea uwezo waganga, watabibu, wavunaji, wakulima, wazalishaji, wauzaji na Watumiaji wa dawa asilia.
Image result for tiba asiliTRAMEPRO kupitia semina, midaharo, makongamano mbalimbali tuliyoandaa na kushirikishwa (kushiriki), vipindi katika redio na television pamoja na mitandao yetu ya kijamii tumejitahidi kuelimisha matumizi sahihi ya dawa asilia na utoaji wa huduma sahihi za tiba asilia kwa matabibu kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa ili kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na uelewa mkubwa juu ya matumizi sahihi ya dawa asili na kulinda mazingira yetu.             
Kwa kutambua Sera, Sheria, Kanuni, taratibu na miongozo inayo simamia shughuri zetu za kila siku na kushirikiana na wadau wa afya na Mazingira  hasa katika kufanya utafiti wa Dutu za mimea,wanyama, madini, ndege na wadudu tutakuza sekta yetu ya Tiba Asilia na Tiba Mbadala.
Leo tumekutana hapa na wadau mbalimbali wa Afya, Tiba Asilia, Tiba Mbadala na mazingira ili kujadili maelekezo na utekelezaji wa Maagizo ya Serikali ya tarehe 15 Januari 2016 yaliyotolewa na Mhe. Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kwa watabibu wa Tiba Asili na Tiba Mbadala, kubadilishana uzoefu, ujuzi na maarifa kati yetu na wadu wengine juu ya njia bora na sahihi za kuwahudumia wagonjwa, ili kupunguza madhara yatokanayo na uzembe, ucheleweshaji na matukio mengine yanayoweza kusababisha ulemavu na vifo.
Pia kutoa elimu nasaha juu ya afya ya msingi kwa wateja wao, na kuleta uhusiano mzuri na wakaribu kwa wote, ikiwa ni pamoja na watabibu wa Tiba Asilia na Tiba Mbadala na jamii yote tukiwa na matarajio ya kuongeza upeo zaidi.
Shirika la dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira TRAMEPRO linaungana katika Mkutano huu ikiwa ni moja kati ya mikutano iliyoshiriki na kuandaa ili kupata maoni ya wadau  na kuongeza upeo zaidi juu ya huduma za Afya zinazotolewa kwa Tiba Asilia na tiba Mbadala na namna ambavyo mazingira yanavyoweza kulindwa.
TIBA ASILI NI NINI?
TIBA ASILI ni Jumla ya maarifa na utendaji ambao unatumika katika kuchunguza, kukinga na kuponya ugonjwa wa kimwili, kiakili au kimahusiano ambao unategemea uzoefu wa kurithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo.



TIBA MBADALA NI NINI?
TIBA MBADALA ni Jumla ya maarifa na utendaji unaotumika katika uchunguzi, ukingaji na uponyaji wa matatizo ya kimwili, kiakili na kijamii na kutegemea tu mifumo mbalimbali iliyoanzishwa na Tiba Mbadala ya Nyanja husika.
Huduma hizi zitolewazo na watu waaina mbalimbali kwa kutumia nyenzo, ujuzi na uzoefu wa kiasili. Tiba asilia hutofautiana toka jamii au kabila moja hadi jingine. Baadhi ya dawa au Tiba toka jamii zingine zina ubora wa kipekee kiasi cha kuleta mvuto sehemu zingine.
MAZINGIRA NI NINI?
Mazingira ni vitu vyote vinavyotuzunguka vyenye uhai na visivyo na uhai. Vitu vyenye uhai ni pamoja na mimea na wanyama na visivyo ni pamoja na uhai ni hewa, ardhi na maji.

Mazingira yanahusisha pia vitu vyote vinavyosaidia kuendelea kuwepo kwa maisha ya mwanadamu na viumbe wengine. Hivyo basi maisha ya viumbe hai wa kizazi kilichopo na kijacho kinategemea uwepo wa mausiano mazuri kati ya watu na mazingira.

KAZI ZA MTABIBU WA TIBA ZA ASILI
Mtabibu wa tiba asili aliyepata mafunzo anatarajiwa kufanya yafuatayo:-
·       Kutunza kumbukumbu za wagonjwa kwa utaratibu unaokubalika.
·       Kutambua na kuhamasisha wagonjwa wenye vidokezo vya hatari na      wanaohitaji rufaa za mapema ili waende kwenye kituo cha afya husika kwa huduma ya utaaramu zaidi.
·       Kutoa huduma salama kwa kujari afya ya mgonjwa huku wakiwa wasafi.
·       Kutoa huduma katika mazingira ya usafi.
·        Kutoa elimu na nasaha kuhusu usafi, lishe bora na utunzaji wa mazingira.
• Kutoa dawa kwa utaratibu unaokubalika
• Kutunza vifaa vya huduma na dawa kwa utaratibu unaokubalika
• Kushirikiana na kuwaelewa watumishi wa afya
• Kupata mwanga juu ya misingi ya utafiti wa madawa ya asili.
• Kushirikiana na mashirika, vikundi vyama mbalimbali hususani vya kitaaluma.
• Kupambanua Watabibu wa kweli na tapeli
• Kutoa ushauri juu ya kupunguza kasi ya kuenea kwa magonjwa hususani magonjwa sugu kama kansa, kisukari, magonjwa ya zinaa na Ukimwi
• Kuzingatia sera, miongozo ya Serikali, sheria na kanuni na taratibu
za kitaaluma.
NAPENDA KUSISITIZA YAFUATAYO
(i) watoa huduma wa tiba asili – wachane na upingaji wa ramri zinazogonganisha/Kuchonganisha jamii na kukosesha amani ndani ya jamii.
(ii) Watoe tiba iliyo na tija kwa jamii ili tuweze kuokoa maisha ya
binadamu kwani watabibu wa tiba asilia mlishapewa karama na mwenyezi
Mungu kuokoa maisha ya watu, hivyo tutowe huduma itakayoendeleza Tiba asilia
(iii) Watabibu wa tiba asilia tunaitaji kuongeza elimu na bidii za utafiti wa madawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana kutibiwa katika jamii zetu.
(iv)Pia wananchi tunaomba nasi tuachane na dhana potofu kwani nasi pia ni chanzo kikubwa cha kuleta ugomvi  kwa sababu unavyokwenda kwa mganga kutibiwa kuna tabia ya kulazimisha waganga wawambie wachawi wenu badala ya kuomba upatiwa dawa stahiki ya kutibu tatizo ulilonalo unayotokana na mimea asilia.

USAFI NA MAZINGIRA
(I) Mtoa huduma wa tiba asili anahitajika kwanza mwenyewe awe msafi wa mwili mzima kabla ya kuanza kazi, nguo zake za kazi ziwe safi, na mazingira yake yawe safi na salama kwa kutolea huduma ya tiba asilia.
Wagonjwa walazwe mahala pasafi, vyombo vya kuifadhia madawa na mahala pa kutunzia madawa pawe pasafi, vifaa viwe safi na salama. Pia anapo fanyia kazi pawe safi, vyoo viwili vyote viwe safi mabafu yote mawili yawe safi, hadi mavazi ya mganga mwenyewe yawe safi.
MADHARA YA UCHAFU
Unapokuwa unatoa huduma ukiwa mchafu basi unaweza kumuongezea mgonjwa wako magonjwa mengine, kumsababishia magonjwa ya kipindupindu, pumu, vikoozi vya kila wakati, ukimwi, pepopunda, funza, upele, ukurutu, kichocho na Ukimwi hatimaye kusababisha vifo vya watu.
WATABIBU TAPELI
Wapo watu wasiokuwa na uelewa juu ya Utoaji huduma ya tiba Aislia wanaodandia na kuchafua jina la taaluma ya tiba asilia ya kitanzania, wapo watu wasiokuwa na taaluma ya tiba asili au wanautambuzi mdogo sana kwa taaluma hii. Wapo wasioijua hii taaluma kazi yao ni kununua dawa kutoka kwa wataaluma, baadaye kujifanya kuwa wenyewe ndiyo wataaluma zaidi.
• Watu hao ni wasemaji sana.
• Hujipa sifa wenyewe
• Hujigamba sana
• Hujikweza
• Husema wana weza kutibu na kuponyesha kila aina ya ugonjwa.
• Ni wadanganyifu mno.
Hizo ni baadhi tu ya dalili za kutambua matapeli na wao wanajipenda sana zaidi ya mganga mwenyewe na gharama zao ni kubwa zaidi.
MAADILI YA TIBA ASILI
Watoa huduma za tiba asilia wanahitaji kuzingatia maadili ya dawa, kazi zao.
(i) Unahitaji kuelewa sera na sheria za 23/2002 ya tiba asili na tiba
mbadala Tanzania.
(ii) Kutunza siri za wateja wako
(iv)Kutokuwa na uongo na udanganyifu.
(v) Kutoendesha shughuli zako kiutapeli
(vi) Kutolewa wakati wa kutoa huduma.
(vii) Kutokubaliana na mteja kulipiza visasi
(viii) Kutopiga ramri za kuchonganisha
(ix) Kutonyanyasa wateja wako na kuwapiga,
(x) Timiza hivyo vipengele utaheshimika sana ndani ya jamii unamoishi.
FAIDA YA DAWA ZA ASILI
1. Inatibu na kuondoa magonjwa sugu
2. Inastawisha afya ya binadam zaidi
4. Ina boresha mwili wa binadam zaidi na ina virutubisho vingi.
Ndugu wananchi tunaomba tuzingatie utamaduni wetu na mila na desturi nzuri tusibaki kuthamini sana mila za kigeni Wananchi tugeuze akili zetu tutumie zaidi dawa zetu za asili ili tuweze kupunguza vifo vingi hapa nchini. Pia tule vyakula vya asili, mfano vyakula vyote vya nafaka na mafuta ya asili, mtaona mabadiliko ya nchi yenu kuwa makubwa kwa afya za binadam hata vifo vitapungua hapa nchini.
Mnaona magonjwa yanazidi kila kunapokucha na tiba hazipo zimebakia za wasiwasi. Nimatumaini kuwa wananchi watabadili fikira zao ili waokowe maisha yao.
Ahsante

IMETAYARISHWA NA KAMATI TENDAJI YA TRAMEPRO
CHINI YA KATIBU MKUU
……………………………
BONIVENTURA F. MWALONGO

KATIBU MKUU

TIBA ASILI TANZANIA NA SHIRIKA LA DAWA ASILIA NA ULINZI WA MAZINGIRA (TRAMEPRO)

TRAMEPRO ni Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (Traditional Medicine and Environmental Protection Organization) lililosajiliwa chini ya Sheria ya Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali yaani Non – Govermental Organization (NGO’s) “Act 24 of 2002” lenye namba ya usajili 00NGO/00007772 linalofanya kazi kwa Karibu na Serikali na Jamii katika kufuatilia Matumizi sahihi ya dawa asilia , uandaaji wa dawa asilia, upatikanaji wa dawa asilia na uvunaji endelevu utakao pelekea kukua kwa pato la mtu mmoja mmoja na uchumi wa nchi pamoja na kulinda Mazingira ili kupata dawa asili iliyo na Virutubisho vya kutosha . Uvunaji makini wa Miti dawa utatuletea upatikanaji wa mvua za kutosha zitakazo tuwezesha katika kilimo, hewa safi, chakula pia kulinda na kuendeleza BAONUAI.

Dira ni kuwa na Jamii yenye kuheshimu, kutumia na kulinda Dawa za Asilia zinazotoka katika mazingira Asili na yaliyolindwa, ili kutuwezesha kuwa na Afya bora, kupambana na adui maradhi nakutambua vyanzo vinavyoweza kuchafua matumizi yetu Salama na kulinda usalama wa watumiaji.

Kwapamoja tunawajibu mbalimbali katika kuangalia upatikanaji na upandaji wa miti dawa ili kupata dawa kwa wingi na kuendelea kulinda Afya zetu na kutunza mazingira yetu. TRAMEPRO tunafanya juhudi mbalimbali za kuhakikisha jamii inapata elimu ya matumizi ya dawa asili na faida zinazopatikana kwa kulinda mazingira yetu .Ili kufanikisha matumizi sahihi ya Dawa asilia na kulinda Mazingira ni muhimu Kutoa Elimu na kuwajengea uwezo waganga, watabibu, wavunaji, wakulima, wazalishaji, wauzaji na Watumiaji wa dawa asilia.

TRAMEPRO kupitia semina, midaharo, makongamano mbalimbali tuliyoandaa na kushirikishwa (kushiriki), vipindi katika redio na television pamoja na mitandao yetu ya kijamii tumejitahidi kuelimisha matumizi sahihi ya dawa asilia na utoaji wa huduma sahihi za tiba asilia kwa matabibu kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyowekwa ili kuhakikisha kuwa jamii inakuwa na uelewa mkubwa juu ya matumizi sahihi ya dawa asili na kulinda mazingira yetu.        
     
Kwa kutambua Sera, Sheria, Kanuni, taratibu na miongozo inayo simamia shughuri zetu za kila siku na kushirikiana na wadau wa afya na Mazingira  hasa katika kufanya utafiti wa Dutu za mimea,wanyama, madini, ndege na wadudu tutakuza sekta yetu ya Tiba Asilia na Tiba Mbadala.

Leo tumekutana hapa na wadau mbalimbali wa Afya, Tiba Asilia, Tiba Mbadala na mazingira ili kujadili maelekezo na utekelezaji wa Maagizo ya Serikali ya tarehe 15 Januari 2016 yaliyotolewa na Mhe. Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kwa watabibu wa Tiba Asili na Tiba Mbadala, kubadilishana uzoefu, ujuzi na maarifa kati yetu na wadu wengine juu ya njia bora na sahihi za kuwahudumia wagonjwa, ili kupunguza madhara yatokanayo na uzembe, ucheleweshaji na matukio mengine yanayoweza kusababisha ulemavu na vifo.

Pia kutoa elimu nasaha juu ya afya ya msingi kwa wateja wao, na kuleta uhusiano mzuri na wakaribu kwa wote, ikiwa ni pamoja na watabibu wa Tiba Asilia na Tiba Mbadala na jamii yote tukiwa na matarajio ya kuongeza upeo zaidi.
Shirika la dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira TRAMEPRO linaungana katika Mkutano huu ikiwa ni moja kati ya mikutano iliyoshiriki na kuandaa ili kupata maoni ya wadau  na kuongeza upeo zaidi juu ya huduma za Afya zinazotolewa kwa Tiba Asilia na tiba Mbadala na namna ambavyo mazingira yanavyoweza kulindwa.

TIBA ASILI NI NINI?
TIBA ASILI ni Jumla ya maarifa na utendaji ambao unatumika katika kuchunguza, kukinga na kuponya ugonjwa wa kimwili, kiakili au kimahusiano ambao unategemea uzoefu wa kurithishwa toka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo.


TIBA MBADALA NI NINI?
TIBA MBADALA ni Jumla ya maarifa na utendaji unaotumika katika uchunguzi, ukingaji na uponyaji wa matatizo ya kimwili, kiakili na kijamii na kutegemea tu mifumo mbalimbali iliyoanzishwa na Tiba Mbadala ya Nyanja husika.
Huduma hizi zitolewazo na watu waaina mbalimbali kwa kutumia nyenzo, ujuzi na uzoefu wa kiasili. Tiba asilia hutofautiana toka jamii au kabila moja hadi jingine. Baadhi ya dawa au Tiba toka jamii zingine zina ubora wa kipekee kiasi cha kuleta mvuto sehemu zingine.
MAZINGIRA NI NINI?
Mazingira ni vitu vyote vinavyotuzunguka vyenye uhai na visivyo na uhai. Vitu vyenye uhai ni pamoja na mimea na wanyama na visivyo ni pamoja na uhai ni hewa, ardhi na maji.

Mazingira yanahusisha pia vitu vyote vinavyosaidia kuendelea kuwepo kwa maisha ya mwanadamu na viumbe wengine. Hivyo basi maisha ya viumbe hai wa kizazi kilichopo na kijacho kinategemea uwepo wa mausiano mazuri kati ya watu na mazingira.

KAZI ZA MTABIBU WA TIBA ZA ASILI
Mtabibu wa tiba asili aliyepata mafunzo anatarajiwa kufanya yafuatayo:-
·       Kutunza kumbukumbu za wagonjwa kwa utaratibu unaokubalika.
·       Kutambua na kuhamasisha wagonjwa wenye vidokezo vya hatari na      wanaohitaji rufaa za mapema ili waende kwenye kituo cha afya husika kwa huduma ya utaaramu zaidi.
·       Kutoa huduma salama kwa kujari afya ya mgonjwa huku wakiwa wasafi.
·       Kutoa huduma katika mazingira ya usafi.
·        Kutoa elimu na nasaha kuhusu usafi, lishe bora na utunzaji wa mazingira.
• Kutoa dawa kwa utaratibu unaokubalika
• Kutunza vifaa vya huduma na dawa kwa utaratibu unaokubalika
• Kushirikiana na kuwaelewa watumishi wa afya
• Kupata mwanga juu ya misingi ya utafiti wa madawa ya asili.
• Kushirikiana na mashirika, vikundi vyama mbalimbali hususani vya kitaaluma.
• Kupambanua Watabibu wa kweli na tapeli
• Kutoa ushauri juu ya kupunguza kasi ya kuenea kwa magonjwa hususani magonjwa sugu kama kansa, kisukari, magonjwa ya zinaa na Ukimwi
• Kuzingatia sera, miongozo ya Serikali, sheria na kanuni na taratibu
za kitaaluma.

NAPENDA KUSISITIZA YAFUATAYO
(i) watoa huduma wa tiba asili – wachane na upingaji wa ramri zinazogonganisha/Kuchonganisha jamii na kukosesha amani ndani ya jamii.
(ii) Watoe tiba iliyo na tija kwa jamii ili tuweze kuokoa maisha ya
binadamu kwani watabibu wa tiba asilia mlishapewa karama na mwenyezi
Mungu kuokoa maisha ya watu, hivyo tutowe huduma itakayoendeleza Tiba asilia
(iii) Watabibu wa tiba asilia tunaitaji kuongeza elimu na bidii za utafiti wa madawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana kutibiwa katika jamii zetu.
(iv)Pia wananchi tunaomba nasi tuachane na dhana potofu kwani nasi pia ni chanzo kikubwa cha kuleta ugomvi  kwa sababu unavyokwenda kwa mganga kutibiwa kuna tabia ya kulazimisha waganga wawambie wachawi wenu badala ya kuomba upatiwa dawa stahiki ya kutibu tatizo ulilonalo unayotokana na mimea asilia.

USAFI NA MAZINGIRA
(I) Mtoa huduma wa tiba asili anahitajika kwanza mwenyewe awe msafi wa mwili mzima kabla ya kuanza kazi, nguo zake za kazi ziwe safi, na mazingira yake yawe safi na salama kwa kutolea huduma ya tiba asilia.
Wagonjwa walazwe mahala pasafi, vyombo vya kuifadhia madawa na mahala pa kutunzia madawa pawe pasafi, vifaa viwe safi na salama. Pia anapo fanyia kazi pawe safi, vyoo viwili vyote viwe safi mabafu yote mawili yawe safi, hadi mavazi ya mganga mwenyewe yawe safi.

MADHARA YA UCHAFU
Unapokuwa unatoa huduma ukiwa mchafu basi unaweza kumuongezea mgonjwa wako magonjwa mengine, kumsababishia magonjwa ya kipindupindu, pumu, vikoozi vya kila wakati, ukimwi, pepopunda, funza, upele, ukurutu, kichocho na Ukimwi hatimaye kusababisha vifo vya watu.

WATABIBU TAPELI
Wapo watu wasiokuwa na uelewa juu ya Utoaji huduma ya tiba Aislia wanaodandia na kuchafua jina la taaluma ya tiba asilia ya kitanzania, wapo watu wasiokuwa na taaluma ya tiba asili au wanautambuzi mdogo sana kwa taaluma hii. Wapo wasioijua hii taaluma kazi yao ni kununua dawa kutoka kwa wataaluma, baadaye kujifanya kuwa wenyewe ndiyo wataaluma zaidi.
• Watu hao ni wasemaji sana.
• Hujipa sifa wenyewe
• Hujigamba sana
• Hujikweza
• Husema wana weza kutibu na kuponyesha kila aina ya ugonjwa.
• Ni wadanganyifu mno.
Hizo ni baadhi tu ya dalili za kutambua matapeli na wao wanajipenda sana zaidi ya mganga mwenyewe na gharama zao ni kubwa zaidi.

MAADILI YA TIBA ASILI
Watoa huduma za tiba asilia wanahitaji kuzingatia maadili ya dawa, kazi zao.
(i) Unahitaji kuelewa sera na sheria za 23/2002 ya tiba asili na tiba
mbadala Tanzania.
(ii) Kutunza siri za wateja wako
(iv)Kutokuwa na uongo na udanganyifu.
(v) Kutoendesha shughuli zako kiutapeli
(vi) Kutolewa wakati wa kutoa huduma.
(vii) Kutokubaliana na mteja kulipiza visasi
(viii) Kutopiga ramri za kuchonganisha
(ix) Kutonyanyasa wateja wako na kuwapiga,
(x) Timiza hivyo vipengele utaheshimika sana ndani ya jamii unamoishi.

FAIDA YA DAWA ZA ASILI
1. Inatibu na kuondoa magonjwa sugu
2. Inastawisha afya ya binadam zaidi
4. Ina boresha mwili wa binadam zaidi na ina virutubisho vingi.
Ndugu wananchi tunaomba tuzingatie utamaduni wetu na mila na desturi nzuri tusibaki kuthamini sana mila za kigeni Wananchi tugeuze akili zetu tutumie zaidi dawa zetu za asili ili tuweze kupunguza vifo vingi hapa nchini. Pia tule vyakula vya asili, mfano vyakula vyote vya nafaka na mafuta ya asili, mtaona mabadiliko ya nchi yenu kuwa makubwa kwa afya za binadam hata vifo vitapungua hapa nchini.
Mnaona magonjwa yanazidi kila kunapokucha na tiba hazipo zimebakia za wasiwasi. Nimatumaini kuwa wananchi watabadili fikira zao ili waokowe maisha yao.
Ahsante

IMETAYARISHWA NA KAMATI TENDAJI YA TRAMEPRO
CHINI YA KATIBU MKUU
……………………………
BONIVENTURA F. MWALONGO

KATIBU MKUU

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *