-

.

.

TRAMEPRO

TRAMEPRO

NAIPENDA NCHI YANGU TANZANIA

Thursday, 27 November 2014

NA HIVI NDIVYO MAONYESHO YA KWANZA YA KIMATAIFA YA TIBA ASILI YA MWAFRIKA YALIVYOKUWA KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

WATAALAMU WA TIBA ASILI WAKUTANA CHINI YA JUKWAA MOJA; WAONYESHA UMAHIRI KATIKA TIBA ASILI NA MBADALA

Mratibu wa Jukwaa la Tiba Asili Tanzania, Boniventura F. Mwalongo akifafanua jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja yalikofanyika Maonyesho ya Tiba Asili na Mbadala


Dr. Jumanne wa Huduma ya Uponyaji akimsikiliza mmoja wa waliotembelea Banda lake kwenye Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Tiba  zinazotolewa na Dk. Jumanne ni zile zinazotokana na Matunda na Mboga Mbalmbali . Simu 0755087303





Dk. Salimu akiwaeleza watu waliofika kwenye maonyesho ya dawa asili jinsi dawa zake zinavyofanya kazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja


Dk.Ahmad Darusi Salimu Mkurugenzi wa M. M.D.K Clinic akitoa maelezo ya jinsi dawa zake zinavyotakiwa kutumika. Yeye amebobea katika kutibu Kansa za aina zote na pia anayo dawa inayosaidia kuondoa magonjwa nyemelezi kwa wagonjwa wa UKIMWI. Simu 0754467406, 0787467406

Mkurugenzi wa Kampuniya Dk.Fadhili Herbal Medicine & Nutritional,akitoa maelezo kwa wateja ((hawapo pichani) waliofika kwenye Banda lake wakati wa Maonyesho ya Tiba za Asili na Mbadala yaliyofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja hivi Karibuni.  Dk. Fadhili pia ni Mshauri wa Afya katika Kampuni ya BF SUMA kutoka Marekani inayojishuhulisha na usambazaji wa dawa zenye Virutubisho vinavyoweza kuongeza kinga ya mwili (CD4) kwa 100%, kurekebisha Sukari na zingine nyingi.  Simu 0713834556

Dk. Nyakubaho (katikati) Mkurugenzi wa Kikundi cha tiba Asili cha Nyakiziba Shunga Tradtional Clinic. Wanazo dawa nyingi za kutibu maradhi mbalimbali kama inavyoonekana Pichani. Simu 0784936177, 0755570321

Bi EmilianaKokuhumuliza, Mtabibu wa asili anayetibu kwa kutumia mitishamba kutoka Mkoa wa Kagera. anapatikana Mjini Morogoro. Simu 0766903297. Picha zote na Muchunguzi Kamugisha wa ZUNGU

mhe.Kingunge Ngombale Mwilu akitembelea moja ya mabanda katika maonesho ya kwanza ya kimataifa ya tiba asili ya mwafrika

























































Sunday, 9 November 2014

BARAZA LA TIBA ASILI, MBADALA LAPIGA MARUFUKU MATANGAZO NA VIPINDI VYA TIBA HIYO

Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Profesa Rogassian Mahunnah.
Kutoka kushoto ni Kaimu Msajili wa tiba Asili Mboni Bakari, Mwenyekiti, Profesa Rogassian Mahunnah na Mfamasia Lucy Samweli.
BARAZA hilo limesema halitambui vipindi na matangazo yote ya tiba asili na tiba mbadala yanayoendelea kwa sasa kwenye vyombo vya habari nchini kwani ni batili yanapotosha na hayana vibali.
Baraza linawaomba wananchi kutokuamini huduma hizo ikiwamo za matumizi ya mashine za Quantim na zile za  kuondoa sumu mwilini, pamoja na  kuwataka waganga wanaotoa tiba hizo kujisajili ili kufanya kazi zao kihalali.
Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Profesa Rogassian Mahunnah alipokuwa akizungmza na wanahabari katika Ukumbi wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.
Kujua mengi zaidi tembela www.boresaclinic.blogspot.com

MWENYEKITI WA TRAMEPRO BWANA SIMBA ABDULRAHMAN SIMBA AKITOA SALAM ZA PONGEZI KWA MHE. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI KWA KUCHAGULIWA KUWA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SEND EMAIL TO TRAMEPRO

Name

Email *

Message *